Saturday, July 7, 2012
Friday, July 6, 2012
Kiungo wa timu ya Mwanza
Kiungo wa timu ya Mwanza,Juma Nyangi(kulia) akiwania mpira na kiungo wa timu ya ManyaraFrank Kijoth,katika mashindano ya vijana U-17 ya Copa Cocacola,kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jana,Manyara ilishinda.Picha na Michael Matemanga
Friday, February 3, 2012
Furaha Maugo
SHABAN Abdallah(27) mkazi wa Gongo la Mboto Mzambaurauni, jijini Dar es salaama anawaomba wasamaria wema kujitokeze kumchangia fedha kwa ajili ya operesheni ya kukatwa mguu unaomsumbua kwa takribani miaka kumi sasa.
Akizungumza jijini Dar es salaam katika ofisi za gazeti hili zilizopo Tabata reline, Abdallah alisema anahitaji jumla ya Sh500,000 hadi 700,000 kwa ajili ya kulipia gharama za operesheni ya kukata mguu mmoja wa kulia unaoonekana kuathirika kutokana na matende matende.
“Nimesumbuka na kuwa mtu wa kulia kila siu kutokana na maumivu ya mguu huu kwa takribani miaka kumi sasa,nimetumia kila aina ya dawa bila mafanikio badala yake mguu unazidi kujaa maji kila kukicha hali inayonisababishia kupata maumivu makali kiasi kwamba wakati mwingine nashindwa kutembea”alisema Abdalla.
Na kufafanua kuwa alianza kuumwa mguu huu mwaka 2001 kwani ulianza kwa dalili za kuwasha lakini kadri siku zinavyoendelea na mguu unazidi kuvimba na kumsababishia maumivu makali.
Hivyo basi kutokana na hali hiyo Shaban alisema inamlazimu kukaa tu nyumbani na kwasasa hana kitu chochote kinachomuingizia kipato wala mtu anayemtegemea kukidhi mahitaji yake ya kila siku wala gharama za matibabu.
‘Mi nadhani suluhisho pekee la mguu huu ni kukatwa na hivi sasa nipo tayari kwa zoezi hili ninachoomba tuwasamarai wema wajitokeze kunichangia fedha a kukijikimu katika operesheni hiyo nikiamini baada ya kupona nitafanya shughuli zangu vizuri”alisema Shabani.
Na kueleza kuwa, Agosti mwaka jana alivyoenda katika hospitali ya Ocean Road ndio aligundulika kuwa na matende na dawa yake ni operesheni ya kupunguza maji au kukatwa mguu kabisa, lakini kutokana na maumivu anayopata ameamua ukatwe kabisa hivyo anawasihi wasamiria wema wamchangie kwa chochote kufanikisha zoezi hilo.
“Gharama za operesheni ya kukata mguu huu hospitali ya Muhimbili nimeambiwa ni Sh 200,000, kipimo cha damu ya usiku Sh 15,000 ,gharama za kupigwa Ultra Sound(Mionzi )ni shilingi 35,000” alisema Abdalla na kufafanua kuwa anaamini kiasi hicho alichoomba kitakidhi mahitaji yake kwa sasa.
Kwa yeyote aliyegushwa na jambo hili anaweza kuwasiliana na Shabani kwa namba 0712 235060 au kumtumia pesa kwa njia ya tigo pesa
Wafungwa
Baadhi ya wafungwa wakiwa chini ya ulinzi kurudishwa Gerezani baada ya kukosa tiba katika Taasisi ya Mifupa MOI jijini Dar es Salaam jana kutokana na mgomo wa Madaktari unaondelea.Picha na Venance Nestory
Wagonjwa
Abdul Benja na Emmanuel Mtuka wakisubiri tiba nje ya Taasisi ya Mifupa MOI jijini Dar es Salaam jana kwa zaidi ya masaa sita hali hiyo inatokana na mgomo wa madaktari unoendelea katika Hosptali ya Taifa ya Muhimbili na baadhi ya vitengo vyake.Picha na Venance Nestory
Subscribe to:
Posts (Atom)